HALMASHAURI
ya serikali ya kijiji cha Kanembwa Runzewe wilaya ya Bukombe mkoani
Geita,imelituhumu jeshi la polisi wilayani humo kujihusisha na rushwa na
ujambazi kutokana na askari wake wa kituo cha Runzewe kudaiwa kuhusika
na mauaji ya mfanyabiashara wa dhahabu Yemuga Fugungu(48).
Mfanyabiashara huyo mkazi wa kitongoji cha Masota anadaiwa kuuawa na polisi hivi karibuni baada ya kumvamia nyumbani kwake na kulipua nyumba yake kwa mabomu na risasi baada ya kumtuhumu kumjeruhi askari mwenzao kwa risasi na kisha kuondoka na mamilioni ya fedha.
Pia askari wawili kati ya 20 waliovamia nyumbani kwa mfanyabiashara huyo wanadaiwa kumfanyia kitendo cha udhalilishaji mke wa marehemu Lucia Kilaza(23)baada ya kumpekua kwa nguvu hadi kwenye sehemu zake za siri na kumvua nguo za ndani kisha kuzichana na kuondoka na sh.1.2 milioni.
Kilaza alikuwa ameficha fedha hizo baada ya askari hao kufika kwenye familia hiyo kisha kuanza kufyatua risasi hewani na kusababisha kifo cha mumewe kilichotokea alhamisi iliyopita.
Awali kamanda wa polisi mkoa wa Geita,Bw.Leonard Paul alisema mfanyabishara huyo alijiua mwenyewe baada ya kumjeruhi askari wa Runzewe Fortunatus Beatus kwa bastola kutokana na askari wa kituo hicho walipokamata gari lake lililokuwa na kokoto zinazodaiwa kuwa ni za wizi.
Madai ya kamanda huyo yamepingwa na ndugu wa marehemu pamoja na viongozi wa serikali ya kijiji hicho ambao wamedai serikali isiwafumbie macho askari hao waliotumia nguvu kupita kiasi na kusababisha kifo na uporaji wa zaidi ya sh.370 milion.
Kauli ya serikali ya kijiji hicho inakuja kufuatia askari hao kwenda kijijini hapo bila kutoa taarifa kwa viongozi wa eneo hilo kitendo ambacho kinadaiwa ni kinyume cha taratibu na sheria,na kimetafasiliwa kuwa ni kujenga mahusiano mabaya kati ya polisi na raia.
Viongozi wa halmashauri hiyo wamesema kitendo cha askari kuingia kijijini hapo bila kutoa taarifa kwa viongozi hao kisha kufanya uharifu, kusababisha kifo na upotevu wa mali hawatofautiani na majambazi.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Masota,Bw.Evarist Mandwa,akizungumzia tukio hilo alisema taarifa za tukio hilo alizipata siku iliyofuata ingawa usiku alisikia milio ya bunduki iliyowashitua wananchi na kushindwa kujitokeza kukabiliana na hali hiyo.
"Hatukuwa na taarifa kama askari wanakuja eneo hili,ndipo kesho yake tulisikia askari wameua na wamepora fedha za marehemu.Hapa kijijini hatuna historia ya marehemu kujihusisha na uhalifu"
Alisema sheria ya serikali inasema kunapokuwa na uharifu eneo husika askari wanapaswa kuonana na uongozi wa mtaa kwa taarifa,kitendo hicho kina hatarisha mahausiano kuwa mabaya kati ya raia na askari.
Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho,Bw.Peter Kuhanda alisema,halmashauri ya kijiji itakutana na kamati ya ulinzi na usalama ya kijiji ili kuandika maelezo kwenda serikali ya mkoa kuitaka iingilie kati kuchunguza nguvu iliyotumiwa na askari hao.
Bw.Kuhanda Alisema tukio hilo limegubikwa na mianya ya rushwa na hivyo kuitaka serikali kuingilia kati suala hilo kwa kuunda tume kuchunguza undani wake ili kuepusha uvunjifu wa amani unaweza kujitokeza kutokana na jazba za wananchi.
Naye diwani wa kata ya Runzewe,Bw.Yusuph Fungameza,alisema serikali isimame kubaini kama nguvu iliyotumika ni halali sambamba na kutoa taarifa sahihi kuhusiana na uchunguzi tukio hilo.
Alisema kwa hali hiyo wananchi watakosa imani na jeshi la polisi ambalo limekuwa likihasisha ulinzi shirikishi jamii kutokana na askari badala ya kulinda haki za raia na mali zake wamegeuka na kuwa wauaji na waporaji wa mali za raia.
"Sikubaliani na kauli ya kamanda wa mkoa wa Geita,kwamba marehemu alimjeruhi askari na kujiua.Kama marehemu alimjeruhi askari kituoni kwa bastola.kwa nini walimruhusi kutoka pale kituoni..tena kwa kutembea,kisha usiku wakamfuata nyumbani kwake,polisi wamehusika moja kwa moja niko tayari kutoa ushahidi"alisema Diwani huyo.
Kutokana na kuwepo kwa hisia tofauti kwa wakazi wa Runzewe kuhusiana na tukio hilo,diwani Fungameza amewataka wananchi wa kata hiyo watulie wakati uchunguzi unaoendelea kabla ya kwenda kudai taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo.
Katika hatua nyingine serikali ya mkoa wa Geita,inatuhumiwa na ndugu wa marehemu kukalia ripoti ya uchunguzi wa jopo la madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa marehemu jumatatu iliyopita.
Mkuu wa mkoa wa Geita,Bw.Said Magalula,ndiyo alipaswa kuitoa ripoti hiyo lakini amekuwa kimya licha ya baadhi ya madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kudai kwamba taarifa hiyo kuwa tayari.
Jumamosi iliyopita ndugu wa marehemu walisusia kuzika mwili wa ndugu yao kwa lengo la kushinikiza majibu ya taarifa ya Bukombe pamoja na kupisha uchunguzi wa mara ya Pili uliofanyika katika hospitali ya wilaya ya Geikta chini ya jopo la madaktari sita kutoka Geita, Bukombe, Mwanza na Dar es Salaam.
- See more at: http://www.jamiiforums.com/blog/polisi-wadaiwa-kumuua-mfanyabiashara-wa-dhahabuwapora-mamilioni-ya-shilingi/#sthash.rKpSaimK.dpuf
Mfanyabiashara huyo mkazi wa kitongoji cha Masota anadaiwa kuuawa na polisi hivi karibuni baada ya kumvamia nyumbani kwake na kulipua nyumba yake kwa mabomu na risasi baada ya kumtuhumu kumjeruhi askari mwenzao kwa risasi na kisha kuondoka na mamilioni ya fedha.
Pia askari wawili kati ya 20 waliovamia nyumbani kwa mfanyabiashara huyo wanadaiwa kumfanyia kitendo cha udhalilishaji mke wa marehemu Lucia Kilaza(23)baada ya kumpekua kwa nguvu hadi kwenye sehemu zake za siri na kumvua nguo za ndani kisha kuzichana na kuondoka na sh.1.2 milioni.
Kilaza alikuwa ameficha fedha hizo baada ya askari hao kufika kwenye familia hiyo kisha kuanza kufyatua risasi hewani na kusababisha kifo cha mumewe kilichotokea alhamisi iliyopita.
Awali kamanda wa polisi mkoa wa Geita,Bw.Leonard Paul alisema mfanyabishara huyo alijiua mwenyewe baada ya kumjeruhi askari wa Runzewe Fortunatus Beatus kwa bastola kutokana na askari wa kituo hicho walipokamata gari lake lililokuwa na kokoto zinazodaiwa kuwa ni za wizi.
Madai ya kamanda huyo yamepingwa na ndugu wa marehemu pamoja na viongozi wa serikali ya kijiji hicho ambao wamedai serikali isiwafumbie macho askari hao waliotumia nguvu kupita kiasi na kusababisha kifo na uporaji wa zaidi ya sh.370 milion.
Kauli ya serikali ya kijiji hicho inakuja kufuatia askari hao kwenda kijijini hapo bila kutoa taarifa kwa viongozi wa eneo hilo kitendo ambacho kinadaiwa ni kinyume cha taratibu na sheria,na kimetafasiliwa kuwa ni kujenga mahusiano mabaya kati ya polisi na raia.
Viongozi wa halmashauri hiyo wamesema kitendo cha askari kuingia kijijini hapo bila kutoa taarifa kwa viongozi hao kisha kufanya uharifu, kusababisha kifo na upotevu wa mali hawatofautiani na majambazi.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Masota,Bw.Evarist Mandwa,akizungumzia tukio hilo alisema taarifa za tukio hilo alizipata siku iliyofuata ingawa usiku alisikia milio ya bunduki iliyowashitua wananchi na kushindwa kujitokeza kukabiliana na hali hiyo.
"Hatukuwa na taarifa kama askari wanakuja eneo hili,ndipo kesho yake tulisikia askari wameua na wamepora fedha za marehemu.Hapa kijijini hatuna historia ya marehemu kujihusisha na uhalifu"
Alisema sheria ya serikali inasema kunapokuwa na uharifu eneo husika askari wanapaswa kuonana na uongozi wa mtaa kwa taarifa,kitendo hicho kina hatarisha mahausiano kuwa mabaya kati ya raia na askari.
Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho,Bw.Peter Kuhanda alisema,halmashauri ya kijiji itakutana na kamati ya ulinzi na usalama ya kijiji ili kuandika maelezo kwenda serikali ya mkoa kuitaka iingilie kati kuchunguza nguvu iliyotumiwa na askari hao.
Bw.Kuhanda Alisema tukio hilo limegubikwa na mianya ya rushwa na hivyo kuitaka serikali kuingilia kati suala hilo kwa kuunda tume kuchunguza undani wake ili kuepusha uvunjifu wa amani unaweza kujitokeza kutokana na jazba za wananchi.
Naye diwani wa kata ya Runzewe,Bw.Yusuph Fungameza,alisema serikali isimame kubaini kama nguvu iliyotumika ni halali sambamba na kutoa taarifa sahihi kuhusiana na uchunguzi tukio hilo.
Alisema kwa hali hiyo wananchi watakosa imani na jeshi la polisi ambalo limekuwa likihasisha ulinzi shirikishi jamii kutokana na askari badala ya kulinda haki za raia na mali zake wamegeuka na kuwa wauaji na waporaji wa mali za raia.
"Sikubaliani na kauli ya kamanda wa mkoa wa Geita,kwamba marehemu alimjeruhi askari na kujiua.Kama marehemu alimjeruhi askari kituoni kwa bastola.kwa nini walimruhusi kutoka pale kituoni..tena kwa kutembea,kisha usiku wakamfuata nyumbani kwake,polisi wamehusika moja kwa moja niko tayari kutoa ushahidi"alisema Diwani huyo.
Kutokana na kuwepo kwa hisia tofauti kwa wakazi wa Runzewe kuhusiana na tukio hilo,diwani Fungameza amewataka wananchi wa kata hiyo watulie wakati uchunguzi unaoendelea kabla ya kwenda kudai taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo.
Katika hatua nyingine serikali ya mkoa wa Geita,inatuhumiwa na ndugu wa marehemu kukalia ripoti ya uchunguzi wa jopo la madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa marehemu jumatatu iliyopita.
Mkuu wa mkoa wa Geita,Bw.Said Magalula,ndiyo alipaswa kuitoa ripoti hiyo lakini amekuwa kimya licha ya baadhi ya madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kudai kwamba taarifa hiyo kuwa tayari.
Jumamosi iliyopita ndugu wa marehemu walisusia kuzika mwili wa ndugu yao kwa lengo la kushinikiza majibu ya taarifa ya Bukombe pamoja na kupisha uchunguzi wa mara ya Pili uliofanyika katika hospitali ya wilaya ya Geikta chini ya jopo la madaktari sita kutoka Geita, Bukombe, Mwanza na Dar es Salaam.
- See more at: http://www.jamiiforums.com/blog/polisi-wadaiwa-kumuua-mfanyabiashara-wa-dhahabuwapora-mamilioni-ya-shilingi/#sthash.rKpSaimK.dpuf
0 comments:
Post a Comment