Msanii wa Uganda, Moses Ssali aka Bebe Cool ameshinda kesi iliyohusu tukio la kufyatuliwa risasi na
polisi miaka mitatu iliyopita, hivyo mahakama kuu ya Uganda imeamua
alipwe kiasi cha pesa za Uganda zenye thamani ya zaidi ya shilingi za
Tanzania milioni 257.
Awali Bebe Cool alifungua mashitaka akidai zaidi ya milioni 533 za Tanzania, kufuatia kujeruhiwa sehemu ya mguu wake.
Bebe
Cool alidai kiasi hicho cha pesa kama fidia ya kipato alichopoteza
katika kipindi cha miezi 9 hadi 12 wakati akiuguza majeraha ya risasi.
Msanii
huyo aliiambia mahakama kuu ya Uganda kuwa alikuwa amepata dili ya
kufanya matangazo na MTN na Century Bottling Co Ltd, makampuni ambayo
yangemlipa kiasi kikubwa cha pesa. Na kuongeza kuwa alikuwa katika
maandalizi ya kurekodi nyimbo 16 kwa ajili ya album yake ambayo
ingemuingizia mkwanja mrefu.
Hata
hivyo, Bebe Cool alishindwa kuwasilisha vielelezo mahakamani kuonesha
hasara hiyo, hivyo mahakama ikaamua alipwe milioni 257 badala ya milioni
533 alizodai.
Bebe
Cool alipigwa risasi January 29 mwaka 2010 na polisi anayejulikana kwa
jina la Anthony Achikan muda mfupi baada ya kupiga show kwenye jukwaa
moja na R.Kelly jijini Kampala.
Bebe
Cool na kundi lake walikuwa barabarani na magari yao mida ya saa tisa
usiku wakielekea Nakumatt, ambapo walikutana na polisi aliyewasimamisha.
Yalitokea
majibishano ya muda mrefu kati ya Polisi huyo na Bebe Cool, ndipo
polisi huyo alifyatua risasi zilizomjeruhi mwimbaji huyo.
Polisi huyo alikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya usalama ambapo alifunguliwa mashitaka kwa kufanya jaribio la kuua.
Polisi huyo alikutwa na hatia na hadi sasa anaendelea kutumikia kifungo cha miaka 9 jela.
0 comments:
Post a Comment