Tuesday, 31 December 2013

Beyonce ajitetea, ni baada ya kutumia sauti ya chombo cha angani kilicholipuka na kuua 7 kwenye wimbo wake XO.


Wajane wa makamanda wa Challenger wamedai kusikitishwa na kitendo hicho cha Beyonce ambaye hata hivyo amesema ametumia sauti hiyo kama heshima kwa makamanda hao.
Wimbo huo uliopo kwenye album yake mpya,'Beyonce' unaanza kwa kusikika sauti ya ofisa wa NASA Steve Nesbitt akisema: "Flight controllers here looking very carefully at the situation. Obviously, a major malfunction."
"Waandishi wa wimbo waliweka sauti hiyo kama heshima kwa kazi ya crew ya Challenger kwa matumaini kuwa hawatasahaulika,” alisema Beyonce kwenye maelezo yake.
"Moyo wangu uko pamoja na familia ya wale waliopoteza maisha kwa janga la Challenger. Wimbo 'XO' ulirekodiwa kwa lengo la wazi kuwasaidia kuwaponya waliopoteza wapendwa wao na kutukumbusha kuwa vitu visivyotarajia hutokea, hivyo penda na kushukuru kila dakika uliyonayo na wale wenye maana kubwa kwako,” alisema Bey.
Baadhi ya mashairi kwenye wimbo huo yanasema:  We don't have forever, Baby daylight's wasting. You better kiss me before our time is run out."

0 comments:

Post a Comment