
Mwimbaji wa Bongo Flava, Barnaba Elias aka Barnaba Boy amepanga kuwatafuta wasanii wawili wapya katika muziki wa kizazi kipya ambao watakuwa chini ya label ya studio yake binafsi aliyopanga kuitambulisha rasmi kwa mashabiki wake.
Mwimbaji
huyo wa ‘Sorry’ ameiambia tovuti ya Times Fm kuwa anahitaji kuwa na
wasanii hao wawili kwa kubalance jinsia, mmoja wa kike na mmoja wa kiume
ambao atasimamia kazi zao za muziki kama meneja wao.
“Kila
kitu kina mipango, kwa sasa nimeshafanya maandalizi ya studio yangu
mpya ambayo soon tu mashabiki wataanza kusikia kazi mbalimbali. Pia
natarajia kusaini wasanii wawili (wa kike na wa kiume) ambao kazi zao
nitakuwa nikizisimamia.” Amesema Barnaba Classic.
“Research yangu nitaianza wakati wowote kuwatafuta wasanii hao wawili hapa Dar es salaam.” Ameongeza.
Hata hivyo, Barnaba amesema bado hajaamua jina litakalowakilisha studio yake na label yake.
0 comments:
Post a Comment