Sunday, 5 January 2014

Britney Spears awachukiza fans waliolipia takribani million 4 kukukutana naye, awapa kila mmoja sekunde 3 tu.

Britney Spears awachukiza fans waliolipia takribani million 4 kukukutana naye, awapa kila mmoja sekunde 3 tuMkali wa Pop, Britney Spears anaripotiwa kuwakwaza mashabiki wake waliokuwa na kiu ya kukutana na kupiga picha
na star huyo, hivyo kulipia $ 2500 (zaidi ya shilingi za kitanzania milioni tatu na laki tisa) ili waweze kuruhusiwa kufanya hivyo nyuma ya jukwaa baada ya show yake huko Las Vegas.
Fans hao waliokuwa wamejipanga kukutana na star huyo na kupiga naye story, walijikuta katika wakati mgumu baada ya kupewa sekunde 3 kwa ajili ya kuweka pozi na kupiga naye picha tu.
“Mashabiki waliambiwa kabla kuwa katika kukutana naye hawaruhusiwi kumgusa wala kumkumbatia bila ruhusa yake na hawakuruhusiwa kumpelekea zawadi yoyote. Na hatimaye walipofanikiwa kukutana naye ilikuwa kama ‘tabasamu, piga picha, kwaheri. Kila mmoja alipata kama sekunde 3 kuwa naye.” Chanzo kimoja kiliuambia mtandao wa Radar Online.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa Britney ni kama hakuongea nao, alikuwa na sentensi moja tu kuwaambia baada ya kupiga picha huku akitabasamu, “Thank-you a lot.”

0 comments:

Post a Comment