
Mwaka 2006, Lady Gaga alikuwa msanii mchanga aliyekuwa akijulikana kwa jina lake Stefani Joanne Angelina Germanotta.
Kipindi
hicho, Germanotta alikuwa na miaka 19 alikuwa akisafiri kwa basi
kutoka New York City kwenda Parsippany, New Jersey siku saba za wiki
kufanya kazi na producer aitwaye Rob Fusari.
Kila
siku Stefani alipokuwa akiingia kwenye studio, Rob alikuwa akicheza
wimbo uitwao ‘Radio Gaga wa Queen, kama wimbo wake wa kuingilia. Siku
moja alikuwa akikuna kichwa kutafuta jina la utani, Fusari akamtumia
sms kupendekeza jina "Radio Ga Ga" lakini masahihisho ya simu
(autocorrect) yakalibadilisha jina na kujiandika "Lady Ga Ga". Stefani
akajibu pale pale: Hilo ndo lenyewe. Hili ndio jina langu jipya.
Usiniite Stefani."
Katika
kipindi hicho ameenza kujiita Gaga, alikuwa akifanya kazi kama
mwandishi wa nyimbo kwenye Streamline records, kampuni ya Jimmy Iovine
wa Interscope records. Stefani aliwaandikia nyimbo wasanii wakubwa
kama Britney Spears na Fergie.
Siku
moja Akon alikuwa akihangaika kuandika nyimbo kwaajili ya albam yake
ya pili "Konvicted". Stefani aliombwa kwenda studio na kuimba sauti
atakazotumia Akon. Akon aliguswa na uimbaji wa Gaga kiasi ambacho
aliacha kurekodi na kwenda moja kwa moja kwenye ofisi ya Jimmy Iovine na
kumshawishi amuachie Stefani amsainishe kwenye label yake Kon Live.
Akon
akaanza kuchangia pia sauti kwenye nyimbo kadhaa za kwenye albam ya
kwanza ya Gaga, "The Fame" na pia alishiriki kuandika wimbo wake wa
kwanza uliomtambulisha, "Just Dance".
Kwenye interview aliyofanya mwaka 2011, Akon alikiri kuingiza fedha kupitia Lady Gaga mara 10 zaidi ya kazi zake mwenyewe.
0 comments:
Post a Comment