Tuesday, 31 December 2013

Kilimo Kwanza: Prince William arudi chuo kusomea masuala ya Kilimo.

Sera ya Tanzania ya Kilimo Kwanza inafanyiwa kazi kivitendo na familia ya kifalme ya Uingereza ambapo Prince William ameamua kurudi chuo kusomea masuala ya kilimo.

Uongozi wa familia hiyo umetoa tamko rasmi jumatatu (December 30), kwamba Prince William atajiunga na chuo kikuu cha Cambridge (Cambridge University) na kusomea maswala ya kilimo kuanzia January hadi March.
“Kozi hiyo imeandaliwa kusaidia kumpa uelewa kuhusu mambo yanayoendelea kutokea yanayoathiri biashara ya kilimo na jamii za vijijini ndani ya  Uingereza.” Utawala huo umeeleza.
Hata hivyo, Prince William ambaye ni baba wa mtoto mmoja ataendelea na majukumu mengine kama kawaida yanayohusu familia hiyo ya kifalme.
Prince William alihitimu shahada ya kwanza ya masomo ya Jografia , St. Andrews University mwaka 2005.
Pia aliwahi kujiunga na mafunzo ya Jeshi na kujikita katika maswala ya uokoaji.

0 comments:

Post a Comment