Tuesday, 31 December 2013

NYERERE, DK. CHENI WAPIGANA VIKUMBO.

www.theclicktz.com

Steve Mangere ‘Steve Nyerere’.
Stori: Nyemo Chilongani
WAIGIZAJI wawili kwenye tasnia ya ya filamu Bongo, Steve Mangere ‘Steve Nyerere’ na Mahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’ wapo katika mvutano wa

hali ya juu kufuatia kila mmoja  kutangaza nia ya kugombea uenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie.
www.theclicktz.comMahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’.
Imeelezwa kuwa, katikati ya wiki iliyopita wasanii hao walikutana katika pati ya Baby Madaha iliyofanyika Posta jijini Dar, ambapo kila mmoja alijinadi kumfunika mwenzake katika nafasi hiyo, hivyo kuzua minong’ono na kuwagawa wasanii, wengine walimuita Steve Nyerere Mwenyekiti, wengine walimuita Dk Cheni.
“Mh! Hivi leo ni vikumbo vya waziwazi maana Steve anajinadi kivyake, mbona hapatoshi tuusubiri huo uchaguzi tuone nani ataibuka kidedea,” alisema msanii mmoja, aliyeomba hifadhi ya jina.

Credit-GPL

0 comments:

Post a Comment